37. Hezro Mkarmeli; Naarai, mwana wa Ezbai;
38. Yoeli, nduguye Nathani; Mibhari, mwana wa Hagri;
39. Zeleki Mwamoni; Naharai Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha wa Yoabu, mwana wa Seruya;
40. Ira na Garebu, waliokuwa Waithri,
41. Uria, Mhiti; Zabadi, mwana wa Ahlai;
42. Adina, mwana wa Shiza Mreubeni, mkuu wa Wareubeni, akiwa pamoja na watu thelathini;
43. Hanani, mwana wa Maaka, Yoshafati Mmithni;
44. Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli, wana wa Hothamu Mwaroeri;
45. Yediaeli na Yoha nduguye, wana wa Shimri Mtizi;
46. Elieli Mmahawi, Yeribai na Yoshavia wana wa Elnaamu; Ithma Mmoabu;
47. Elieli, Obedi, na Yaasieli Mmesobai.