43. Yesu akamjibu, “Nakuambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
44. Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likaifunika nchi yote mpaka saa tisa,
45. na pazia lililokuwa limetundikwa hekaluni likapasuka vipande viwili.
46. Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47. Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”