20. Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
21. Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
22. Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANATHA – BWANA, NJOO!
23. Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24. Upendo wangu uwe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.